Toleo la Bibilia Linganisha

1
Yesu akaingia kwenye chombo, akavuka na kufika katika mji wa kwao.
2
Wakati huo huo wakamletea mtu aliyepooza, akiwa amelazwa kwenye kitanda. Yesu alipoona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, jipe moyo mkuu, dhambi zako zimesamehewa.”
3
Kwa ajili ya jambo hili, baadhi ya walimu wa sheria wakasema mioyoni mwao, “Huyu mtu anakufuru!”
Swahili Bible 2025
Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015 na Biblica, Inc
1
Isa akaingia kwenye chombo, akavuka na kufika katika mji wa kwao.
2
Wakati huo huo wakamletea mtu aliyepooza, akiwa amelazwa kwenye mkeka. Isa alipoiona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, jipe moyo mkuu. Dhambi zako zimesamehewa.”
3
Kwa ajili ya jambo hili, baadhi ya walimu wa Torati wakasema mioyoni mwao, “Huyu mtu anakufuru!”
Swahili Bible 2024
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc
1
Isa akaingia kwenye chombo, akavuka na kufika katika mji wa kwao.
2
Wakati huo huo wakamletea mtu aliyepooza, akiwa amelazwa kwenye mkeka. Isa alipoiona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, jipe moyo mkuu. Dhambi zako zimesamehewa.”
3
Kwa ajili ya jambo hili, baadhi ya walimu wa Torati wakasema mioyoni mwao, “Huyu mtu anakufuru!”
Swahili Bible 2018
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™
1
Yesu akapanda katika mashua na akasafiri kwa kukatisha ziwa kurudi kwenye mji wake.
2
Baadhi ya watu wakamletea mtu aliyepooza akiwa amelala kwenye machela. Yesu alipoona imani waliyokuwa nayo, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Changamka mtoto wangu! Dhambi zako zimesamehewa.”
3
Baadhi ya walimu wa sheria walisikia alichosema Yesu. Wakaambizana wao kwa wao, “Si anamtukana Mungu mtu huyu akasema hivyo!”
Swahili Bible 2017
Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi Toleo la Awali © 2017 Bible League International
1
Akapanda katika mashua, akavuka, akafika mjini kwao.
2
Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, akiwa amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako.
3
Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru.
Swahili Bible 2013
The Holy Bible in Kiswahili, Revised Union Version © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 2013
1
Akapanda chomboni, akavuka, akafika mjini kwao.
2
Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako.
3
Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru.
Swahili Bible 2005
Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005
1
Yesu akaingia katika chombo akavuka tena ziwa kwenda upande wa magaribi, naye akafika katika muji wake.
2
Na kule wakamuletea mutu mwenye ugonjwa wa kupooza, akilala juu ya kipoyi. Yesu alipoona namna watu wale walivyomwaminia, akamwambia yule mwenye kupooza: “Mutoto wangu, ujipe moyo! Zambi zako zimesamehewa!”
3
Halafu walimu wamoja wa Sheria waliokuwa pale wakajisemesha: “Mutu huyu anamutukana Mungu!”
Swahili Bible 2002
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002
1
Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake.
2
Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako.”
3
Baadhi ya waalimu wa sheria wakaanza kufikiri, “Mtu huyu anamkufuru Mungu!”
Swahili Bible 2001
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki - 1995, 2001
1
Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake.
2
Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako.”
3
Baadhi ya waalimu wa sheria wakaanza kufikiri, “Mtu huyu anamkufuru Mungu!”
Swahili Bible 1995
Swahili Common Language DC Bible: Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki © Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya, 1995, 2001. Haki zote zimehifadhiwa
1
Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake.
2
Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako.”
3
Baadhi ya waalimu wa sheria wakaanza kufikiri, “Mtu huyu anamkufuru Mungu!”
Swahili Bible 1993
Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993 The Bible Society of Kenya 1993
1
Akapanda chomboni, akavuka, akafika mjini kwao.
2
Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako.
3
Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru.
Swahili Bible 1952
Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
1
*Akaingia chomboni, akavuka, akafika mjini mwake yeye.
2
Papo hapo wakamletea mgonjwa wa kupooza aliyelala kitandani. Yesu alipoona, walivyomtegemea, akamwambia mwenye kupooza: Tulia, mwanangu! Makosa yako yameondolea.
3
Ndipo, waandishi waliokuwako waliposema mioyoni: Huyu anambeza Mungu.
Swahili Bible 1937
Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937
1
AKAPANDA chomboni, akavuka, akafika mjini kwake.
2
Wakamletea mgonjwa wa kupooza, amelala kitandani: na Yesu, akiona imani yao, akamwambia yule mgonjwa wa kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanaugu; umeondolewa dhambi zako.
3
Baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru.
Swahili Bible 1921
Swahili New Testament © Bible Society of Tanzania, 1921
1
Yesu alipanda mashua, akavuka ziwa na kufika katika mji wake.
2
Hapo watu walimletea mtu mmoja aliyepooza mwili, amelazwa juu ya kitanda. Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, “Jipe moyo mwanangu! Umesamehewa dhambi zako.”
3
Baadhi ya walimu wa Sheria wakaanza kufikiri, “Mtu huyu anamkufuru Mungu!”
Swahili Bible 1850
Portions of the New Testament in the Swahili Language of Kenya, Mozambique, Somalia, and Tanzania, translation by Dr. Johann Ludvig Krapf completed in 1850